Tuesday 25 March 2014

Wazazi yampongeza JK


Jumuia ya Wazazi ya CCM, imempongeza Rais Kikwete, kwa kutoa hotuba iliyozungumzia mambo muhimu kuhusu mustakabali wa taifa.
Katibu wa Wazazi, Seif Shaban Mohamed, alisema jana kuwa hotuba hiyo ilikuwa na mambo mazito, ambayo Watanzania wengine walikuwa hawafahamu.
“Tunaunga mkono hotuba ya Rais Kikwete kwa kuwa imefunua macho Watanzania wengi, kazi iliyobaki ni kwa wajumbe wa bunge kukaa na kuweka utaifa mbele ili tupate katiba,” alisema.
Alisema Rais Kikwete alihimiza mshikamano, amani na utulivu katika kupata katiba mpya, ambayo rasimu yake itajadiliwa na wajumbe.
Katibu alisema hotuba hiyo ilikuwa na mambo yenye uwazi na ukweli kwa kuzungumzia athari zilizojificha katika muundo wa serikali tatu
Kamati namba moja: 
Ummy Mwalimu (Mwenyekiti)
Profesa Makame Mbarawa (Makamu)
Kamati namba mbili :
Shamsi Vuai Nahodha (Mwenyekiti)Shamsa Mwangunga (Makamu)
Kamati namba tatu:
Francis Michael (Mwenyekiti)
Fatuma Mussa Juma (Makamu)
Kamati namba nne :
Christopher Ole Sendeka (Mwenyekiti)
Dk. Sira Ubwa Mwamboya (Makamu)
Kamati namba tano:
 Hamad Rashid Mohammed (Mwenyekiti)
Assumpter Mshama (Makamu)
Kamati namba sita:
Stephen Wasira (Mwenyekiti) 
Dk. Maua Abeid Daftari (Makamu)

Kamati namba saba:
Hassan  Ngwilizi (Mwenyekiti)
Waride Bakari Jabu (Makamu)
Kamati namba nane:
Job Ndugai (Mwenyekiti)
Biubwa Yahya Othaman (Makamu)
Kamati namba tisa: 
Kidawa Hamid Salehe (Mwenyekiti)
William Ngeleja (Makamu)
Kamati namba 10: 
Anna Abdalla (Mwenyekiti) 
Salmin Awadhi Salmin (Makamu)
Kamati namba 11:
 Anne Kilango Malecela (Mwenyekiti)
Hamad Massaun (Makamu)
Kamati namba 12: 
Paul Kimiti (Mwenyekiti) 
Sheiba Kisasi (Makamu)


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru