Thursday 24 October 2013

Dk. Sheni hakuna linaloshindikana


Na Mwandishi Wetu, Zanzibar
RAIS wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Sheni, amesema hakuna lisilowezekana katika kuleta maendeleo lakini jambo la msingi ni wananchi kujiamini na kuwa na dhamira ya kweli ya kuendeleza nchi yao.
Aliyasema hayo jana wakati akizungumza katika mahojiano maalum na Kamati ya Uandishi wa Taarifa za Serikali kuhusu Miaka 50 ya Mapinduzi yaliyofanyika ofisini kwake Ikulu.
ìHakuna lisilowezekana katika kubadili maendeleo yetu kuwa bora zaidi lakini kwanza tunapaswa kujiamini kuwa tunaweza kufanya hivyo na kudhamiria,î alisema Dk.Sheni.
Aliongeza kuwa Wazanzibari wanapaswa kubadilika kwa kufanya mambo yao kwa malengo na kwa wakati na kunukuu kauli ya Rais wa kwanza wa Zanzibar, Marehemu Abeid Amani Karume kuwa la leo ni lazima lifanywe leo.
ìTumezoea kusubiri kuhimizwa na wakati mwingine mawizarani hatupendi hata kuona wengine wanafanyakazi. Nchi za wenzetu wanafanyakazi kwa dhamira na wanapata maendeleo. Tukibadilika nasi tutakuwa kama wenzetu,î alisema Dk. Sheni.
Alibainisha kuwa jitihada zimekuwa zikifanywa na serikali kuwapeleka watumishi wake nchi mbalimbali kujifunza ili kutumia uzoefu wa nchi hizo kusukuma maendeleo ya nchi.
Kuhusu mafanikio ya miaka 50 ya Mapinduzi, Dk. Sheni, alisema wananchi wa Zanzibar wameshuhudia mafanikio katika sekta mbalimbali ambapo huko nyuma baadhi walibeza lakini hivi sasa wamekubali.
ìTumepata mafanikio makubwa katika sekta mbalimbali za maendeleo wako waliokuwa wakiyabeza lakini sasa wamekubali kuwa Zanzibar tumepiga hatua kubwa katika maendeleo,î alisema.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru