Thursday 24 October 2013

Kampuni yakamatwa ikisambaza mbolea feki


Na Mwandishi Wetu
MAMLAKA ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA), imekamata zaidi ya tani 2,700 za mbolea feki ya kupandia aina ya CAN yenye thamani ya zaidi ya sh.bilioni mbili.
Mbolea hiyo, iliyoelezwa na TFRA kuwa ilimaliza muda wake wa matumizi tangu mwaka jana, ilikuwa ikisafirishwa kinyemela kwenda katika mikoa ya Nyanda za Juu Kusini, ambayo ni maarufu kwa kilimo cha mazao ya chakula.
Aidha, TFRA imechukua uamuzi mzito wa kuinyangíanya kampuni ya Swiss Singapore Overseas Enterprises PTE Limited, leseni ya  kufanya biashara hiyo, sanjari na kulifunga ghala lake lililopo eneo la Tabata Matumbi, Manispaa ya Ilala, Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mkuu wa TFRA Dk.Susan Ikerra, alisema katika eneo la tukio wakaguzi wake walifanikiwa kupata taarifa kuhusu hujuma zinazofanywa na kampuni hiyo, kwa kusambaza mbolea feki kwa wakulima.
Dk. Suzan alisema wamiliki wa kampuni hiyo walikutwa wakisimamia uchekechaji wa mbolea hiyo ambayo haifai kwa matumizi ya kilimo na iliyoganda kama mawe ya kujengea nyumba na kuitenganisha.
Alisema mmoja wa maofisa wa kampuni hiyo waliihadaa mamlaka yake kwa kuandika barua na kuomba kibali cha kutaka kubadilisha mifuko ya mbolea hiyo kutokana na kupata dhoruba na hivyo kuchanika ikisafirishwa kutoka bandarini.
“Lakini kumbe nia yao haikuwa njema kwa TFRA, bali walitaka kutumia kibali chetu ili kuhalalisha madhambi haya ya kutenganisha mbolea iliyoganda na kuichekecha na kisha kuiweka tena kwenye mifuko na kuisambaza,î alisema Dk. Suzan.
Mkurugenzi huyo wa TFRA aliwaoonyesha waandishi wa habari waliokuwa eneo la tukio moja ya magari lenye namba T723 AXR na T247 AWG mali ya Abinel Mahepela wa Njombe, yaliyokuwa tayari yamepakiwa mbolea hiyo kupelekwa kwa wakulima wa mkoa wa Njombe.
Hata hivyo, wakijitetea mbele na Mkurugenzi wa TFRA na maofisa waandamizi wa idara ya Ukaguzi, wakiongozwa na Samson Mussa, wawakilishi wa kampuni hiyo Manish Kothari na Santosh Reddy, walidai tatizo s

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru