Tuesday 22 October 2013

Fastjet bado yang’ang’aniwa



NA MWANDISHI WETU
MAMLAKA ya Viwaja vya Ndege Tanzania (TCAA), imeiagiza kampuni ya ndege ya Fastjet kukutana leo na mfanyabiashara Majaliwa Mbasa ili wamalize mgogoro wao.
Kwa mujibu wa barua ya TCCA iliyosainiwa na James Mabala kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, iliitaka Fastjet kukutana na Mbasa kwa lengo la kupata suluhu kutokana na kusudio la kushitakiwa mahakamani kwa kukatisha mkataba baina yake na mteja huyo (Mbasa).
Mabala, ameutaka uongozi wa Fastjet kufika katika Ukumbi wa Mamlaka hiyo uliopo katika Jengo la Mamlaka ya Anga, saa tatu asubuhi.
Mbasa anakusudia kuifikisha Fastjet mahakamani kufuatia kushindwa kumsafirisha kutoka Dar es Salaam hadi Johannesburg, Afrika Kusini.
Kampuni hiyo iliahirisha safari muda mfupi kabla ya kuondoka, kitendo ambacho Mbasa amedai kimevuruga mipango yake na kumsababishia hasara.
Anataka arejeshewe gharama za tiketi ya safari ambazo ni sh. 521,560 pamoja na dola za Marekani 5,000 (sh. milioni nane), kama fidia kutokana na usumbufu.
Oktoba 9, mwaka huu, TCAA iliitaka kampuni hiyo kumaliza mgogoro huo ndani ya siku saba, lakini ilishindwa kufanya hivyo na sasa imeamua kuingilia kati kwa lengo la kupata suluhu.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru