Thursday 31 October 2013

Lukuvi, Chiku ngoma nzito


SERIKALI imesema imeweka mpango kamambe kuhakikisha kuwa tatizo la maji katika Jimbo la Isimani mkoani Iringa linaondoka kabisa.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Uratibu na Bunge, William Lukuvi, aliyasema hayo jana bungeni alipokuwa akitoa ufafanuzi wa tatizo hilo kufuatia swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Chiku Abwao (CHADEMA)
Chiku, alisema jimbo hilo limekuwa na matatizo makubwa ya maji kwa muda mrefu na hivyo, alitaka kujua mkakati wa serikali katika kulitatua tatizo hilo.
“Mimi ni msemaji wa serikali, naweza kujibu swali lolote kama hamjui na kwa taarifa tu, tatizo la maji katika jimbo hilo ambalo mimi ni mbunge wake linashughulikiwa kwa nguvu kubwa,’’ alisema Lukuvi baada ya kupewa nafasi.
Lukuvi, alisema serikali inalifahamu tatizo la maji katika Jimbo hilo na tayari mradi mkubwa wa maji katika Jimbo hilo wenye thamani ya sh. Bilioni 3 umeanza kutekelezwa.
“Mimi nikiwa kama mbunge wa Jimbo hilo la Isimani kwa kupitia vyanzo vyangu mbalimbali, nimesha chimba visima 25 katika jimbo hilo na tunaendelea kuchimba vingine 10,’’ alisema Lukuvi.
Alisema nia ni kuhakikisha kila kijiji katika jimbo hilo kinakuwa na kisima kitakachikuwa kikitoa maji muda wote.
Swali hilo la Chiku, lilikuwa ni la nyongeza kwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu), Stephen Wasira, kuhusiana na miradi inayotekelezwa na TASAF.


Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru