Wednesday 27 August 2014

JK kukutana na vyama vya siasa


Katika hatua nyingine, Rais Kikwete, anatarajiwa kukutana na viongozi wa vyama vinayounda Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD).
Mwenyekiti wa TCD, John Cheyo, alisema jana kuwa Rais Kikwete atakutana na viongozi wa vyama hivyo wiki hii baada ya ombi lao kukubaliwa.
Viongozi hao waliazimia kutafuta nafasi  ya kuonana na Rais Kikwete kwa lengo la kushauriana naye na tunashukuru amekubali na tutakutana naye wiki hii, alisema Cheyo.
TCD inaundwa na vyama vyenye uwakilishi bungeni ambavyo ni CCM, UDP, CHADEMA, CUF, NCCR Mageuzi, TLP na UPDP ambacho hakina uwakilishi bungeni. 
Hata hivyo, hakuwa tayari kutoa maudhui wala mahali patakapofanyika kikao hicho zaidi ya kupongeza Rais Kikwete kukubali ombi hilo.
Bunge la Katiba lawaka 
BUNGE Maalumu la Katiba, limewajia juu waandishi wa habari kwa kile walichoeleza kuwa wamepotosha taarifa zake.
Mkurugenzi wa Habari na Itifaki wa Bunge hilo, Jossey Mwakasukya, alisema jana wakati akitoa ufafanuzi wa baadhi ya taarifa kuwa wabunge hao hawajlipwa kwa siku 10.
Alisema habari hizo ni upotoshaji mkubwa tofauti na taarifa zilizotolewa na Katibu wa Bunge hilo na kuwa wajumbe wote walishapata baadhi ya malipo na mengi yalitarajiwa kufanyika juzi.
Alisema iwapo kuna ucheweshaji wa malipo basi  hutokana na sababu maalumu za kiserikali kwani, kila malipo hufuata taratibu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru