Thursday 28 August 2014

Spika Makinda ataka ushirikiano Bunge la EAC


Na Mwandishi Wetu
SPIKA wa Bunge, Anne Makinda, amewataka wabunge wa Bunge la Afrika Mashariki (EALA) kutengeneza utaratibu wa kuongeza uhusiano kati ya bunge hilo na yale ya nchi wanachama.

Akizungumza katika ufunguzi wa bunge hilo, Spika Anne alisema tayari maspika wa mabunge ya nchi wanachama wa Jumuia ya Afrika Mashariki (EAC), wamekubalina kuunda kamati zitakazoshughulikia mambo ya jumuia hizo.

“Lakini jambo kubwa ni kwamba ukanda huu umetengeneza bunge lenye uwezo wa kutunga sheria, mikataba na kusimamia masuala mbalimbali, hivyo kusababisha nchi za afrika kufuata utaratibu huo,” alisema Makinda.
Alisisitiza kuwa Maspika wa nchi za Afrika wamekubaliana kuunda Bunge la Afrika litakalokuwa kamili, ambalo wabunge wake watachaguliwa kama wanavyopatikana wa bunge la EALA na kutaka kuimarishwa zaidi ili kuendelea kuwa mfano.
Akizungumzia mgogoro wa kumuondoa Spika wa Bunge hilo, Mwenyekiti wa Wabunge wa Tanzania katika bunge hilo, Adam Kimbisa, alisema mjadala huo umefungwa kisheria na kinachoendelea ni migogoro ya kisiasa tu.
Kimbisa alisema katika kikao hicho cha wiki mbali watajadili amsuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na viwnago vya elimu kwa nchi zote kumuwezesha mtu kuajilika katika nchi hizo pamoja na mabadiliko ya hali ya hewa.
Naye Naibu Waziri wa Afrika Mashariki, Dk Abdulla Juma Saadalla alisema Tanzania kuwa wa kwanza kukubali umoja wa fedha kwa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki ni kunatokana na umoja huo kuwa na faida kwa wananchi wa Tanzania.
“Sio kweli kuwa Tanzania tunachelewesha mambo isipokuwa lazima tufanye kwa uamakini kama hili la umoja wa foroza tumepeleka bungeni na kukubalika baada ya kueleza faida kwa nchi na wananchi wake,” alisema.
Aliongeza kuwa ni lazima kuwa na shirikisho lenye faida na kutoa mfano wa matumizi ya vitambulisho kuingia katika nchi hizo ambayo Tanzania ilitaka vitumike vya kielektroniki na siyo vya shule.

Alisema sasa nchi zote zimeanza mchakato wa kuwa na vitambulisho hivyo, huku Tanzania tuliokuwa wa mwisho tumeishaanza kutoa kwa 
wananchi wake hivyo kuonesha kwa jinsi nchi ilivyo makini.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru