Saturday 23 November 2013

Lema njia panda


NA SHAABAN MDOE,ARUSHA.
UMOJA wa Vijana wa CCM (UVCCM) mkoa wa Arusha, umemweka njia panda Mbunge wa Arusha Mjini (CHADEMA), Godbles Lema, kwa kumuuliza tangu lini amemtambua Meya wa Jiji hilo, Gaudance Lyimo(CCM) hadi  kushiriki kumchagua Naibu Meya kutoka chama chake, Prosper Msofe.
Swali hilo linatokana na mbunge huyo kuwa mstari wa mbele kupinga kuchaguliwa katika nafasi ya naibu meya aliyekuwa diwani wa Kimandolu (CHADEMA), Estomii Mallah aliyefukuzwa uanachama na wenzake wane.
Akizungumza katika mkutano uliofanyika kwenye viwanja vya soko kuu la Arusha, <wenyekiti wa UVCCM mkoa wa Arusha, Robson Meitinyiku, alisema Lema anapaswa kuwaeleza muafaka gani alioupata katika jambo hilo lililogharimu maisha ya watu hadi kukubali kufanyika kwa uchaguzi huo wa naibu meya hivi karibuni.
“Wananchi lazima tuamke sasa na tuwe na uthubutu wa kuhoji, yeye alisababisha ndugu zetu kupoteza maisha hapa katika maandamano ya kumpinga meya huyu huyu aliyehudhuria kikao kilichoongozwa naye na kumchagua naibu meya halafu tunakaa kimya tu. Mtu akikwambia jambo analojua ni la kijinga akijua ni la kijinga na wewe ukalifanya atakudharau sana,” alisema.
Meitinyiku alisema yeye alikuwa mmoja wa wananchi  waliokuwa wakisubiri kwa hamu majibu ya maswali mengi katika mkutano alioufanya hivi karibuni kuhusu ahadi zilizotolewa na mbunge huyo ikiwemo ya kumpinga meya kwa kuwa alidai uchaguzi uliomuweka madarakani haukuwa halali.
Alisema kutokana na mbunge huyo kutokuwa na majibu sahihi juu ya ushiriki wake kumpigia kura naibu meya kutoka chama chake, kunaonyesha ubaguzi wa wazi na hofu ya nafasi yake ya ubunge dhidi ya Mallah.
Mbali na swali hilo lililotarajiwa na wananchi, alisema pia Lema alitarajiwa kujibu swali na lini atajenga Machinga Comlex aliyoiahidi, hospitali ya akina mama yenye bwawa la kuogelea, kuhamisha kituo cha mabasi ya mikoani, kutoa mikopo kwa wajasiriamali na wapi alipopeleka gari la wagonjwa na trekta alilopewa na wahisani.
Alisema matarajio hayo yote yaliyeyuka katika mkutano huo baada ya kuonekana akizungumzia zaidi masuala ya picha zake chafu zilizozagaa katika mitandao ya kijamii akipeleka tuhuma hizo kwa UVCCM na mgogoro wake na aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
“Alichotakiwa kukifanya ni kueleza fedha za mfuko wa jimbo alivyozitumia katika kuwakwamua kiuchumi vijana, wanawake na wakazi wa jimbo lake kwa ujumla badala ya kubaki kuzitumia fedha kwa manufaa yake au kuziacha bila kuzifanyia kazi na wananchi wakikosa msaada hata wa mikopo.
Akijibu tuhuma za kuzagaa kwa picha zake chafu, alisema Lema anapaswa kujifungia chumbani na wenzake na kutafakari kwa kina namna picha hizo zilivyopatikana na kisha kusambazwa katika mitandao hiyo, kwa kuwa jumuiya yake ina kazi nyingi za kufanya kwa vjana na wananchi na si kukimbizana naye.
Naye katibu wa WAZAZI Mkoa wa Arusha, Rehema Mohamed, alisema Lema hapaswi kutafuta mchawi katika mambo yaliyomkuta kwa kuwa hizo ni mbegu chafu alizozipanda  mwenyewe kwa madai ya kuwajengea wananchi ujasiri.
Alisema kwa kipindi kirefu Lema amekuwa akiwachochea na kuwagombanisha wananchi na viongozi wa serikali yao hadi kufikia kuwafundisha ukosefu

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru