Tuesday 19 November 2013

Polisi yamteua Athumani Hamis


NA JESSICA KILEO
JESHI la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, limemteua aliyekuwa Mpigapicha Mkuu wa gazeti la HabariLeo, Athuman Hamis, kuwa balozi wa uzinduzi wa kampeni ya usalama barabarani kuelekea mwisho wa mwaka.
Kampeni hiyo imeanzishwa kutokana na changamoto ya ajali za barabarani zinazotokea kwa wingi mwishoni mwa mwaka na kusababisha madhara maklubwa ya vifo, ulemavu wa kudumu, uharibifu wa mali na miundombinu.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo jana mjini Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Pereira Ame Silima ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Usalama Barabarani, alisema, wamemteua balozi huyo katika kampeni hiyo ili kupunguza wimbi la ajali.
Silima alisema kwa kuwa Hamisi ni muhanga wa ajali za barabarani, wanaamini atatoa elimu kwa watumiaji wa aina zote wa barabara na kukubalika kwa kuwa anayo picha ya njia zinazosababisha ajali.
Hamisi ambaye amekuwa mlemavu wa viungo baada ya kupata ajali ya gari miaka mitano iliyopita, anatarajiwa kuongoza kampeni hiyo ili kuelimisha jamii juu ya madhara ya ajali hiyo.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru