Tuesday 19 November 2013

Nchi masikini kususia mikutano ya kimataifa


NA RAMADHANI MKOMA, WARSAW, POLAND
NCHI zinazoendelea zimetishia kujitoa katika mikutano ijayo ya kimataifa ya mabadiliko ya hali ya hewa, iwapo mataifa yaliyoendelea yataendelea kusuasua kutoa fedha kusaidia nchi masikini kukabiliana na athari zake.
Hayo yalijitokeza katika mkutano wa Kamati ya Mawaziri wa Mazingira kutoka Afrika uliofanyika juzi, ikiwa ni maandalizi ya Mkutano wa 19 wa Kimataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa unaofanyika mjini hapa.
Waziri wa Nchi Ofisi za Makamu wa Rais (Mazingira), Dk. Terezya Huviza, alizasema hayo alipokuwa akizungumzia vikao vya awali vya maandaliazi ya mkutano huo, unaofanyika katika Uwanja wa Taifa wa Warsaw mjini hapa.
Hata hivyo, Terezya alisema kilio cha mawaziri hao kitawasilishwa kwa marais wa Afrika kupitia kwa Rais Jakaya Kikwete ili kuzungumza na viongozi wa mataifa makubwa ili kushawishi watekeleze ahadi zao kwa mataifa masikini.
Rais Kikwete atawasilisha kilio hicho akiwa ni Rais wa Kamati za Mazingira katika Umoja wa Afrika. Rais Kikwete aliwasili mjini hapa jana.
Kwa mujibu wa Dk. Terezya ambaye ni Rais wa Mawaziri wa Mazingira Afrika, mataifa yaliyoendelea yana kila sababu za kufidia mataifa masikini kutokana kuwa wazalishaji wakuu wa hewa ukaa ambayo imekuwa ikichangia kwa kiwango kikubwa mabadiliko hayo.
Alisema Afrika inachangia asilimia tatu tu za hewa ukaa, licha za madhara na athari kubwa inazokumbana nayo kutokana na mabadiliko ya hali za hewa.
Waziri huyo alisema matukio za mafuriko, mmomonyoko katika maeneo za fukwe ya bahari yanachangiwa kwa kiasi kukubwa na mabadiliko hayo ya hali za hewa.
Kutokana na hilo, Terezya amewataka Watanzania kujikita katika upandaji wa miti itakayosaidia kunyonya hewa ukaa na kupooza bahari na hivyo kuepuka mawimbi makubwa yanayoweya kusababisha mafuriko.
Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Kwanza ya Rais, Zanzibar, Fatma Ferej, alisema athari za mabadiliko ya hali ya hewa zimeanza kujionyesha visiwani humo, ambapo baadhi ya maeneo ya fukwe yameliwa na bahari.
Pia, alisema utafiti uliofanywa umebaini kuwepo kwa maeneo zaidi ya 100 ambayo ardhi yake imemegwa na bahari na hivyo kutishia shughuli za kilimo kutokana na maeneo hayo kuwa na chumvi.
Fatma alisema katika maeneo hayo, wananchi wamekuwa wakipata ugumu wa kupata maji safi ya kunywa kutokana na kuwepo kwa kiwango kikubwa cha chumvi.
Kwa mujibu wa Fatma, mabadiliko hayo ya hali ya hewa yameanza kuathiri miundombinu, ikiwemo kuharibika kwa baadhi ya madaraja kutokana na kuliwa na maji chumvi.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru