Friday 19 July 2013

JK mgeni rasmi Siku ya Mashujaa


Na Mwandishi Wetu
RAIS Jakaya Kikwete anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa.
Taarifa iliyotolewa jana, mjini Dar es Salaam na Ofisi ya Waziri Mkuu, Maadhimisho na Sherehe za Kitaifa, ilisema maadhimisho hayo yatafanyika Julai 25, mwaka huu.
Maadhimisho hayo kitaifa yatafanyika mkoani Kagera katika makaburi ya Kaboya.
Taarifa hiyo ilisema shughuli zitakazofanyika ni gwaride na uwekaji silaha katika mnara wa mashujaa.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo, kutakuwa na dua kutoka kwa viongozi wa madhehebu mbalimbali ya dini nchini.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru