Wednesday 28 May 2014

Dovutwa alazwa Aga Khan


NA MWANDISHI WETU
MJUMBE wa Bunge Maalumu la Katiba na Mwenyekiti Chama cha UPDP, Fahmi Dovutwa, amelazwa katika Hospitali ya Aga Khan kutokana na kusumbuliwa na matatizo ya kifua.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa UPDP, Felix Makuwa jana ilisema kuwa,
Dovutwa alilazwa juzi hospitalini hapo baada ya kusumbuliwa na maradhi ya kifua kwa siku kadhaa.
“Alianza kusumbuliwa na kifua tangu wiki iliyopita. Tatizo hilo limekuwa likimsababishia pumzi kuziba,îalisema.
Makuwa alisema awali, Dovutwa alikwenda katika Hospitali ya Sanitas Mikocheni, lakini kutokana na hali yake kuwa mbaya, alihamishiwa Aga Khan.
Alisema bado hali ya kiongozi huyo si nzuri na kwamba, amehamishiwa katika Chumba cha Uangalizi Maalumu (ICU), ambako madaktari wanaendelea kumtibu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru