Sunday 25 May 2014

Viwanda vya kukamulia alizeti kujengwa Singida

NA MWANDISHI WETU, SINGIDA
SERIKALI mkoani Singida, imesema inatarajia kujenga viwanda vitano vya kukamulia mafuta ya alizeti.

Mkuu wa mkoa huo, Dk. Paraseko Kone alisema hayo juzi katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana inayoendelea mkoani Singida.

Alisema kati ya viwanda hivyo, vinne vitakuwa vya kati na kimoja kitakuwa kikubwa katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati, ambacho kitajengwa mjini hapa.

Dk. Kone alisema lengo la ujenzi wa viwanda hivyo ni kuongeza thamani ya zao la alizeti na kupata soko la uhakika la zao hilo.

Alisema katika mwaka 2006/2007, tani 28 za alizeti zilizalishwa katika mkoa huo na kwamba msimu uliopita walizalisha tani 200,000.

Kwa upande wake, mmoja wa wamiliki wa kiwanda cha kukamulia mafuta ya alizeti, Yussuf Amiri, alisema wananchi wa mkoa huo wana mwamko mkubwa wa kulima zao la alizeti.

Kwa upande wake, Kinana alisema Mkoa wa Singida unaongoza kwa kujenga viwanda vidogo vya kukamulia mafuta ya alizeti.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru