Wednesday 28 May 2014

Wanafunzi bora wapewa fedha badala ya vocha


NA MWANDISHI WETU
WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, imetoa ufafanuzi kuhusu zawadi zilizotolewa kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mtihani wa kumaliza elimu ya msingi na sekondari, mwaka jana.
Imesema wanafunzi 10 wa kidato cha nne walipewa vocha za thamani ya sh. 500,000 kwa ajili ya kununua vitabu vya kiada na ziada.

Shukuru Kawambwa - Waziri (MoEVT)

Taarifa hiyo ilisema wizara imeamua kuwakabidhi wanafunzi 10 wa kidato cha nne fedha taslimu sh. 500,000 badala ya vocha, ili wanunue vitabu wao wenyewe.
“Hii ni kwa sababu wanafunzi hawa wanaweza kujiunga na kidato cha tano katika tahasusi mbalimbali na ni vyema wakanunua vitabu kulingana na tahasusi zao,”alisema.
Taarifa hiyo iliyotolewa jana na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Profesa Sifuni Mchome, ilisema katika kilele cha maadhimisho ya wiki ya elimu, kilichofanyika Mei 10, mwaka huu, mkoani Dodoma, tuzo mbalimbali zilitolewa, zikiwemo za fedha kwa makundi tofauti.
Ilisema tuzo ya fedha taslimu ilitolewa kwa wanafunzi 30, waliofanya vizuri katika mtihani wa mwaka jana, ambapo wanafunzi watano bora, waliofanya vizuri katika mtihani wa elimu ya msingi, walipata sh. 120,000.
Profesa Mchome alisema wanafunzi watano bora wasichana na wanafunzi bora wavulana waliofanya vizuri mtihani wa kumaliza kidato cha nne, walipata sh.250,000.
Sifuni Mchome - Katibu Mkuu (MoEVT)

Alisema pia kuwa, wanafunzi watano bora wasichana na watano bora wavulana waliofanya vizuri katika mitihani ya taifa ya kumaliza elimu ya sekondari kitado cha sita, walipata sh. 500,000.
Kwa mujibu wa Profesa Mchome, fedha zngine zilizotolewa, zilikuwa ni hundi ya sh. milioni tatu  kwa walimu wa shule 60 zilizoongoza ufaulu katika mtihani wa mwaka jana.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru