Tuesday 23 September 2014

Arusha kupandisha kiwango cha ufaulu

NA LILIAN JOEL ARUSHA
HALMASHAURI ya Jiji la Arusha kupitia mpango wa matokeo makubwa (BRN), inatarajia kupandisha kiwango cha ufaulu kwa mwaka 2014, hadi kufikia asilimia 92  kwa elimu ya msingi.
Takwimu zinaonyesha katika matokeo ya mwaka jana, ufaulu ulikuwa asilimia 85.
Hayo yalisemwa juzi na Ofisa ElimuTaaluma wa Shule za Msingi katika halmashauri ya Jiji hilo, Mbwana Juma, alipokuwa akizungumza wakati wa mafunzo ya  mbinu za kufundisha masomo ya hisabati na sayansi.
Alisema  kupitia BRN wanatarajia ufaulu mwaka huu kupanda
hadi kufikia asilimia 92,

“Elimu hii tunatoa kwa walimu wa shule za serikali ambapo kwakushirikiana na Chama cha Walimu Tanzania(CWT), tunawapa walimu mbinuza kufundisha, ili tuongeze ufaulu zaidi kwani tunatoa elimu ya mazingira pia, ” alisema.
Awali Katibu wa CWT  Jiji la Arusha, Magreth Hovokela, alisema
mafunzo hayo ambayo yametolewa kwa walimu 92 kutoka katika shule zote
46 za Msingi zilizopo jijini hapa, yalianza kutolewa tangu mwaka 2000.
Hivi sasa mpango huo umeendelea katika mikoa ya Kilimanjaro na Manyara. Mafunzo hayo yanayofadhiliwa na Shirika la Helvetos, la Uswis.
Aliiomba serikali  isaidie ili mradi huo ufike katika mikoa yote nchini katika kuhakikisha watoto wanaokuwa na nafasi sawa.
Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Uhuru, Zulina
Rajabu, alisema  mafunzo hayo yamewasaidia kujifunza namna ya
kushirikisha wanafunzi wakati wa ufundishaji.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo, Mwalimu Roselyn Mosha, kutoka Shule ya Msingi Sinoni, alisema kuwa mafunzo hayo yanawasaidia kuboresha namna ya ufundishaji na kuiomba serikali kuboresha zaidi sekta ya  elimu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru