Wednesday 17 September 2014

Meli ya matibabu kuzinduliwa Mwanza


NA MWANDISHI  WETU, MWANZA
MRADI wa meli ya huduma za matibabu, ulio chini ya  Dayosisi ya Africa Inland Church Tanzania (AICT), mkoani hapa, unatarajiwa kuzinduliwa hivi karibuni.
 Askofu Mkuu Dayosisi ya Geita, Musa Magwesela, alisema meli hiyo inatarajia kutoa huduma za matibabu katika visiwa mbalimbali vilivyopo ndani ya ziwa Victoria na mikoa ya Geita, Kagera na Mwanza.
Alisema Ziwa Victoria lina takribani visiwa 90 huku, vikikisiwa kuwa na wakazi wapatao 450,000.
 “Kupitia meli hiyo, huduma ya matibabu zitawafikia wakazi hao kwa urahisi na kutolewabila malipo yoyote, alisema.”
Magwesela alieleza kuwa meli hiyo iligharimu kiasi cha sh. bilioni 2.5 za kitanzania na madaktari watakuwa wakitibu magonjwa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na meno, huduma za uzazi kwa wanawake na wanaume, chanjo, afya ya mtoto, kinga na kutoa elimu ya afya.
Alisema meli hiyo ina vyumba viwili vya madaktari, vitanda 18 kwa ajili ya wafanyakazi na sehemu ya kupumzikia wagonjwa zaidi ya 40.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru