Tuesday 9 September 2014

Jela miaka 15 kwa shambulio la aibu


NA SOPHIA ASHERY, A3
MAHAKAMA ya Wilaya ya Ilala imemhukumu Hassan Seleman (23), kifungo cha miaka 15 jela kwa kosa la shambulio la aibu.
Hukumu hiyo ilitolewa jana na Hakimu Juma Hassan baada ya mahakama  kuridhishwa na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo.
Karani wa mahakama hiyo, Felister Mosha, alidai kuwa Seleman alitenda kosa hilo Oktoba 23, mwaka jana, maeneo ya Kitunda Migombani, jijini  Dar es Salaam.
Felister alidai kuwa Seleman alimchukua mtoto wa miaka mitatu (jina linahifadhiwa), aliyekuwa akitoka shule na kwenda naye nyumbani kwao na kisha kumuingizia vidole sehemu za siri.
Akisoma hukumu hiyo, Hakimu Hassan alisema ametoa adhabu hiyo kwa kuwa kitendo kilichofanywa na mshitakiwa ni cha kulaaniwa.
Alisema adhabu hiyo ni fundisho kwa mshitakiwa pamoja na wengine ambao wamekuwa wakifanya vitendo kama hivyo vya aibu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru