Wednesday 17 September 2014

JK awapandisha saba JWTZ


NA MWANDISHI WETU
AMIRI Jeshi Mkuu, Rais Jakaya Kikwete amewapandisha vyeo Maofisa saba  wa Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), kutoka cheo cha Brigedia hadi kuwa Meja Jenerali.
Hatua hiyo aliitekeleza kwa mujibu wa kanuni za majeshi ya ulinzi ya Tanzania ambazo zinatambulika kisheria.
Maofisa waliopandishwa vyeo ni Brigedia Jenerali Gaudence Milanzi, Brigedia Jenerali James Mwakibolwa, Brigedia Jenerali Ndetaulwa Zakayo na Brigedia Jenerali Venance Mabeyo.
Wengine ni Brigedia Jenerali Simon Mumwi, Brigedia Jenerali Issa Nassor na Brigedia Jenerali Rogastian Laswai, ambao wamekuwa na vyeo vya Meja Jenerali kuanzia Septemba 12, mwaka huu.
Katika tafrija ya kuwavisha vyeo vipya maofisa hao, iliyofanyika makao makuu ya jeshi eneo la Upanga, Dar es Salaam, Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, Jenerali Davis Mwamunyange, alimwakilisha Rais Kikwete.
Uteuzi huo pia umempandisha Meja Jenerali Gaudence Milanzi kuwa Mkuu wa Chuo cha Ulinzi wa Taifa (NDC).
Meja Jenerali Milanzi amechukua nafasi hiyo baada ya kustaafu kwa aliyekuwa Mkuu wa Chuo hicho,  Luteni Jenerali Charles Makakala.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru