Tuesday 9 September 2014

Kizimbani kwa ubakaji


NA EMMANUEL MOHAMED
MKAZI wa Dar es Saalam Juma Omary, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni kujibu shitaka la ubakaji.
Omary (65), alisemewa shitaka hilo jana, mahakamani hapo na Mwendesha Mashitaka Faustine Sylvester mbele ya Hakimu Boniphace Lihamwike.
Sylvester alidai kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Agosti 19, mwaka huu, muda usiofahamika, katika mtaa wa Mkunguni, Kinondoni.
Mshitakiwa alikana shitaka hilo na alirudishwa rumande, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Hakimu Lihamwike alimtaka awe na wadhamini wawili,
ambao watumishi wa Serikali. Kesi itatajwa Septemba 22, mwaka huu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru