Tuesday 9 September 2014

Umekwapua simu? Sasa utakiona


NA EMMANUEL MOHAMED
MATHIAS Abdallah (64), mkazi wa Kinondoni, Dar es Salaam, amefikishwa katika Mahakama ya Mwanzo ya Kinondoni kwa kosa la wizi wa simu ya mkononi.
Karani Alfred Lengalenga alidai mbele ya Hakimu Hakimu Anna Kihiyo kuwa mshitakiwa alitenda kosa hilo Jumapili iliyopita maeneo ya Mwananyamala. Alidai kuwa aliiba simu aina ya Samsung Note 3 na Nokia Obama, zenye thamani ya sh. milioni moja, mali ya Mzurimwema.
Mshitakiwa alikana mashitaka hayo, na kumlazimu Hakimu Kihiyo kumsomea masharti ya dhamana kutokana na kutokamilika kwa upelelezi wa kesi hiyo.
Hakimu Anna alimtaka mshtakiwa awasilishe mahakamani hapo wadhamini wawili, wenye ajira za kudumu watakao tia saini ya bondi ya sh. 500,000.
Mshitakiwa alirudishwa rumande,kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana. Kesi itatajwa tena Septemba 19, mwaka huu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru