Tuesday 9 September 2014

Vijisenti vyamfikisha kortini


SOMOE NKHOMEE, TUDARCO
MKAZI wa Dar es Salaam, Ally Mohammed, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mwanzo Kariakoo, akikabiliwa na shitaka la wizi wa sh. 55,000.
Mohammed (22), alifikishwa mahakamani hapo juzi na kusomewa shitaka na karani Lucy Rutabanzibwa, mbele ya Hakimu Mkazi Christina Luguru.
Lucy alidai mshtakiwa alitenda kosa hilo Septemba 4, mwaka huu, saa nane alasiri maeneo ya soko la samaki la Ferry, wilayani Ilala.
Alidai mshitakiwa aliiba sh 55,000 mali ya Khadija Hussein, aliyefika sokoni hapo kwa ajili ya kununua samaki.
Mshtakiwa alikiri shitaka hilo na kurudishwa rumande hadi Septemba 11, mwaka huu, baada ya kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Mshitakiwa alitakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye barua kutoka serikali ya mtaa na kila mmoja kutia saini ya bondi ya sh 200,000.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru