Thursday 11 September 2014

Raisi Kikwete akutana na Yoweri Museveni


NA MWANDISHI WETU
RAIS Jakaya Kikwete, amefanya mazungumzo ya faragha na mgeni wake, Rais Yoweri Museveni wa Uganda, Ikulu, Dar es salaam.
Rais Museveni ambaye alikuwa kwenye ziara ya siku moja ya kikazi katika Tanzania, aliwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 4:10 asubuhi na kupokelewa na Rais Kikwete.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu, mazungumzo kati ya viongozi hao wawili, yalianza saa 5:30 asubuhi na kuchukua kiasi cha saa 1.15.
Rais Museveni aliondoka Ikulu baada ya chakula cha mchana na aliagana na mwenyeji wake, Rais Kikwete kwenye uwanja wa JNIA, kabla ya kupanda ndege yake kurejea nyumbani.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru