Wednesday 17 September 2014

Wawili wapoteza maisha Ubena Senge


NA MWAMVUA MWINYI, KIBAHA
WATU wawili wamekufa na wengine 25 wamenusurika baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso katika eneo la Ubena Senge, Bagamoyo, barabara kuu ya Morogoro.
Ajali hiyo ilitokea jana, saa 12.15 asubuhi, baada ya gari aina ya Toyota Coaster no.T 663 BKP, kugongana na gari la mafuta, aina ya Leyland lenye namba T858 CLK na tela T 421 CKY, mali ya kampuni ya Ramader . Gari hilo lilikuwa likitokea  jijini Dar es Salaam kwenda Morogoro.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, Athumani Mwambalasa, alisema gari la mafuta lilikuwa likiendeshwa na dereva Rashid ambaye alitoroka mara baada ya ajali hiyo.
Kamanda huyo aliwataja waliofariki dunia kuwa ni Neema Mile (39) na Jane Mtani (38), wote wakazi wa Dar es Salaam.
Alisema  majeruhi walipelekwa katika hospitali ya Tumbi mkoani Pwani.
Mwambala alisema chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dereva wa coaster baada ya kuhama upande wake.
Dereva huyo anashikiliwa na  polisi.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru