Thursday 18 September 2014

Silima: Ajali ni janga la taifa


NA MWANDISHI WETU
SERIKALI imesema kwa sasa inawekeza zaidi katika mapambano dhidi ya ajali za barabrani kutokana na idadi kubwa ya Watanzania kupoteza maisha.
Imesema kwa sasa ajali zimekuwa janga la taifa kuliko hata ugonjwa wa Ukimwi, hivyo jitihada za haraka zinahitajika katika kudhibiti.
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani, Pereira Ame Silima, aliyasema hayo  jana  alipokuwa akipokea hundi ya  sh. milioni 40 kutoka kwa Kampuni ya Puma, kwa ajili ya Maadhimisho ya Wiki ya Nenda  Usalama Barabarani.
Hata hivyo, alisema kuwa wimbi la ajali hizo haimaanishi kwamba, serikali na Jeshi la Polisi zimelala, bali mikakati madhubuti inaendelea kuchukuliwa ili kukomesha kabisa.
Pia alisema kuanzia sasa utoaji wa leseni kwa madereva wa mabasi yote ya mikoani utazingatia mafunzo ya kutosha kwa wahusika wote.
Alitumia fursa hiyo kuwataka madereva kuwa makini na kuwa uzembe na uamuzi usio makini barabarani, ikiwemo ulevi, mwisho wake ni mbaya na kuwa sheria itachukua mkondo wake.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru