Wednesday 17 September 2014

Kagera yazindua kampeni ya kuimarisha Chama


NA  ANGELA SEBASTIAN, BUKOBA.
CHAMA  Cha Mapinduzi (CCM) mkoani hapa, kimezindua rasmi kampeni ya kuimarisha Chama ili kujiweka sawa na kujihakikishia ushindi wa kishindo katika uchaguzi ujao.
Uzinduzi wa kampeni hizo uliofanyika jana, katika kata za Ruhunga na Kyaitoke wilayani Bukoba vijijini, ulikwenda sambamba na ugawaji wa vifaa kama bendera, milingoti na kamba ikiwa ni hatua mojawapo ya kufufua kazi za mabalozi.
Akizungumza katika uzinduzi huo, Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya  CCM (NEC), Nazir Karamagi, alisema vifaa hivyo vitakabidhiwa kwa mabalozi wote 5,520, na kwa wenyeviti wa matawi na kata.
Karamagi alisema kuwa mabalozi ni jeshi muhimu katika mapambano na kuwa haiwezekani  kuwaacha bila kuwapa nyenzo wakati wanategemewa katika Chama.
Naye katibu wa CCM Bukoba vijijini, Acheni Maulid, alisema mabalozi wamekuwa wakilalamika kuwa wanakumbukwa wakati wa uchaguzi na ndiyo maana CCM imeamua kuitisha mikutano ya mabalozi katika wilaya.
“Hii maana yake tunawatambua na kuwathamini,” alisema Maulid.
Karamagi anafanya ziara ya wiki mbili katika wilaya hiyo kwa lengo la kuzungumza na mabalozi na viongozi wengine wa Chama.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru