Wednesday 23 July 2014

‘Tuna imani na Askofu Massangwa’


NA LILIAN JOEL, ARUSHA
WAUMINI wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Kaskazini Kati, wamesema  Askofu Mteule Solomon Massangwa ni chaguo la Mungu na hawana shaka naye.
Massangwa alichaguliwa juzi, kuwa Askofu wa Dayosisi hiyo baada ya kupata kura 261 kati ya kura 263, sawa na asilimia 99.98 na msaidizi wake,  Mchungaji Gidion Kivuyo alipata kura 242 kati ya kura 263.
Uchaguzi huo ulifanyika juzi, katika Shule ya Sekondari Peace House iliyoko Kata ya Mtevesi wilayani, Arumeru.
Muunini wa dayosisi hiyo Methew Mollel alisema wajumbe waliompigia kura Massangwa wametimiza sauti ya Mungu kwa kuwa na imani kubwa na mteule huyo bila ya kutia shaka yoyote katika utendaji kazi wake.
Alisema anaimani kubwa sana na utendaji kazi wake kwani kwa kipindi cha siku zaidi ya 532 amekuwa akikaimu nafasi hiyo na amefanya mambo makubwa, ikiwa ni pamoja na kuwanganisha waumini wa kanisa hilo.
Askofu huyo amechaguliwa kuziba nafasi iliyoachwa na Askofu Thomas Laizer, aliyefanyika dunia Februari 6 mwaka huu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru