Wednesday 25 March 2015

CCM imeleta maendeleo Moshi Vijijini- Chami



MBUNGE wa Moshi Vijijini, Cyril Chami, amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimeleta maendeleo makubwa katika jimbo hilo tangu kiliposhika madaraka.
Chami alisema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Mikocheni,   katika ziara ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana.
Alisema awali jimbo hilo lilikuwa likiongozwa na viongozi kutoka vyama vya upinzani kwa muda wa miaka 10.
Chami alisema katika kipindi hicho chote, hakuna maendeleo yaliyopatikana, jambo ambalo linaoonyesha kuwa wapinzani hawana uwezo wa kuleta maendeleo kwa wananchi.
Alisema katika kipindi chake cha uongozi, jimbo hilo limepiga hatua kubwa, ikiwa ni pamoja na ujenzi wa shule za sekondari na maabara.
Ilielezwa kuwa  shule mbili za sekondari zilijengwakatika  kila kata na kufanya idadi ya shule kuwa 39.
Mbunge huyo alisema hali hiyo inatokana na kutumika vizuri kwa Mfuko wa Maendeleo wa Jimbo, ambao kwao kipaumbele ni elimu.

"Katibu mkuu, hapa sisi tumeweka kipuambele chetu kuwa ni elimu, hivyo mfuko wa jimbo pamoja na fedha zangu na wafadhili wetu, tumezielekeza huko,” alisema.

Chami alimlalamikia diwani wa CHADEMA kwakuzusha uongo kuwa mbunge huyo hajafana jambo lolote la maendeleo.
Akizungumza katika mkutano huo Kinana aliwataka wakazi wa kata hiyo kuachana na maneno ya wapinzani kwani kazi yao ni maneno.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru