Monday 16 March 2015

Taarifa ya tume kuchunguza operesheni tokomeza yaiva



NA RACHEL KYALA
TUME ya Uchunguzi wa Operesheni Tokomeza, inatarajia kuwasilisha taarifa yake kwa Rais Jakaya Kikwete, wakati wowote kuanzia sasa.
Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji (mstaafu) Hamisi Msumi, alisema hayo alipozungumza na Uhuru jana na kueleza kwamba wameshakamilika kazi.
Alisema walifanya majumuisho ya taarifa na kukamilisha ripoti ambayo  wanapaswa kumkabidhi Rais Kikwete.

“Wakati wowote kuanzia leo, tutamwomba Rais Kikwete atupangie siku ya kukutana naye ili tumkabidhi ripoti hiyo. Kwa kuwa yeye ndiye mwenye shughuli nyingi, atatupangia nafasi na sisi tuko tayari,” alisema.

Tume hiyo iliundwa na Rais Kikwete, Mei mwaka jana, ili kuchunguza, kukusanya na kupokea taarifa juu ya malalamiko juu ya mwenendo wa utekelezaji wa  Operesheni Tokomeza Ujangili nchini, hususan katika mikoa ya Arusha, Manyara, Tabora, Singida na Dodoma.
Hatua ya Rais Kikwete ya kuunda tume hiyo ilitokana na baada ya operesheni hiyo iliyoanza Oktoba 2013, kusitishwa na Bunge Novemba 4, 2013, kutokana ukiukwaji wa sheria na haki za binadamu wakati wa utekelezaji wake.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru