Monday 16 March 2015

ZIARA YA KATIBU MKUU WA CCM Arusha - Komrade Abdulrahman Kinana

KATIBU Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana (katikati) akishiriki kupaka rangi nyumba ya mganga wa hospitali ya kijiji, iliyojengwa na wanakijiji cha Bulati. Wengine ni mbunge wa Ngorongoro,
Kaika Ole Telele (kulia) na Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Arusha, Onesmo Ole Nangole.

NAPE akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Nainokanoka.

KINANA akizungumza na Nape kabla ya kuhutubia wananchi wa kijiji cha Nainokanoka, kilichoko wilaya ya Ngorongoro mkoani Arusha.

KINANA akikaribishwa kwa ngoma za kiasili za kabila la Kimasai, kabla ya kuanza kwa mkutano katika kijiji cha Nainokanoka

KATIBU Mkuu wa CCM, Kinana na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, wakiongozana na wananchi kwenda kijiji cha Nainokanoka, ambako alihutubia mkutano wa hadhara.

KATIBU Mkuu wa CCM, Kinana akihutubia wananchi wa kijiji cha Nainokanoka, ikiwa sehemu ya ziara yake ya kuimarisha  Chama na kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi. (Picha zote na Adam Mzee).

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru