Monday 16 March 2015

Kigoda atoa kauli nzito



NA REHEMA MAIGALA
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk. Abdallah Kigoda amewataka wajasiriamali wanaoanza biashara zao wasiwe wanalipishwa kodi mpaka baada ya miaka mitatu.
Amesema kuwalipisha kodi wajasiriamali hao kunasababisha biashara zao kutoendelea na kutofikia malengo waliyojiwekea katika uendelevu wa biashara na maendeleo kwa jumla.
Akizungumza na Uhuru jana  jijini Dar es Salaam, Dk. Kigoda alisema kuwalipisha kodi wajasiriamali ambao ndio kwanza wanaanza, kunawaharibia malengo yao.

“Tuige mfumo wa nchi ya Malaysia ambao mjasiriamali akianza biashara yake hatakiwi kulipishwa kodi mpaka baada ya miaka mitatu.

Alisema  suala la wajasiriamali kutolipa kodi atalipeleka mbele ya bunge ili liweze kujulikana kwa uwazi.
Dk. Kigoda alisema wanatarajia kuanzisha viwanda mama ili vijana waweze kupata ajira za kudumu na kwamba viwanda hivyo vitakaa kwa muda mrefu kwa kuwa vitakuwa na bidhaa za kudumu.

Kuna Maoni 0 mpaka sasa.

Toa Maoni Yako Kwa Uhuru